Maafisa wawili wa Umoja wa Mataifa leo wameelezea hofu yao juu ya hali nchini Ivory Coast , na kusema baadhi ya viongozi wanachagiza ghasia na chuki miongoni mwa jamii na kuonya kwamba wanaohusiaka watawajibishwa chini ya sheria za kimataifa.
Watu 2700 wamefariki dunia kwa kipundupindu nchini Haiti kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA.
Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wanaohusika na masuala ya majanga wameongeza nguvu kusaidia shughuli za uimarishaji hali ya maisha kwa mamia ya wananchi wa Colombia ambao wameathiriwa vibaya na mafuriko.
Mradi wa kuwapa wanawake mafunzo ambao hawana uwezo wa kupata ajira uliofadhiliwa na shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR umetajwa kuwa wenye manufaa kwa familia zao.
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP linasema kuwa limetumia karibu dola milioni sita mwaka huu kuwasaidia watu 240,000 waliothirika na mizozo kusini mwa Kyrgzstan na wengine 340,000 katika mikoa sita kati ya mikoa saba nchini humo.
Bodi ya wakurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP imeidhinisha kuongeza mwaka mmoja zaidi ya mpango wa msaada wa chakula nchini Bangladesh.
Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa nchini Afghanistan Staffan De Mistura amelaani vikali shambulio la bomu lililotegwa barabarani hii leo na kulipua basi la abiria kwenye mji wa Hahr-s-Saraj wilaya ya Helmand.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM limesema upungufu wa chakula, ukosefu wa ajira na huduma za afya ni changamoto kubwa inayowakabili wanawake wa Iraq ambao ni wakimbizi wanaorejea nyumbani na kuwa na jukumu la kuangalia familia zao.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumiwa watoto UNICEF nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limekuwa likianisha kazi za ofisi yake katika mji wa Lubumbashi ambayo ni kupambana ukosefu wa uelewa wa kutosha miongoni mwa watu wa kuzuia virusi vya HIV na ukimwi.
Rais Omar al Bashir wa Sudan amesema serikali yake itajitoa kwenye mazungumzo na kundi la waasi wa Magharibi mwa Darfur endapo hakunakuwa na muafaka ifikapo mwisho ya siku ya leo Alhamisi Desemba 30.