Taarifa iliyotolewa na kundi la pande nne kwa ajili ya mashariki ya Kati Quartet linalojumuisha Umoja wa Mataifa, Urusi, Marekani na muungano wa Ulaya inasema inaunga mkono mazungumzo ya ana kwa ana baina ya Israel na Palestina ili kupata suluhu ya kudumu ya amani.