Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema, mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita (ICC) imefanikiwa kulazimisha serikali kubadili mwelekeo wao tangu iundwe miaka minane iliyopita.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametoa wito wa kufanyika uchunguzi dhidi ya shambulio la boti iliyobeba misaada kupeleka Gaza na kukatili maisha ya watu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema linahitaji dola milioni 17 ili kukabiliana na kuzuka kwa surua, kipindupindu na homa ya matumbo nchini Zimbabwe.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo ameelezea umuhimu wa kupunguza hatari za majanga katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa na kufikia malengo ya kuzitoa nchi zinazoendelea katika umasikini.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye amekuwa nchini Malawi katika sehemu ya kwanza ya ziara yake barani Afrika baada ya kukutana na Rais Bingu wa Mutharika alihutubia.
Wawakilishi wa serikali 20 za mataifa yaliyo watu wengi walioambukizwa Ukimwi barani Afrika wanakutana Nairobi kujadili jinsi ya kukomesha maambukizi ya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ifikapo 2015.