Ripoti mpya ya mabadiliko ya tabianchi ni historia ya zahma kubwa: UN
Ripoti mpya ya shirika la utabiri wa hali ya hewa la Umoja wa Mataifa WMO, iliyotolewa leo Jumapili, inaonyesha kuwa miaka minane iliyopita imekuwa ya joto zaidi katika historia ya rekodi, ikichochewa na kuongezeka kwa viwango vya gesi chafuzi.