Skip to main content

Chuja:

WMO

13 OKTOBA 2022

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

-Dunia ipo hatarini kuingia katika mwaka mwingine wenye uhaba wa chakula wakati huu ambapo watu wengi tayari wanazidi kuingia katika dimbwi la uhaba wa chakula, limeonya shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani WFP ambalo limetoa wito wa hatua za haraka kuchukuliwa kushughulikia mzizi wa tatizo hili wakati dunia ikielekea kuadhimisha siku ya chakula duniani hapo Oktoba 16.

Sauti
12'35"

11 OKTOBA 2022

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

-Umoja wa Mataifa umeshtushwa na ongezeko kubwa la wakimbizi wa ndani huko magharibi kwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC baada ya kuibuka kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe mwezi Julai huko Kwamouth.

Sauti
10'44"

08 SEPTEMBA 2022

Katika jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa, Flora Nducha anakuletea 

-Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa Maendeleo UNDP kuhusu maendeleo ya binadamu inaonyesha kuwa maendeleo hayo ya binadamu ynashuka kwa karibu asilimia 90 ya nchi duniani

Sauti
13'15"
Mabadiliko ya tabianchi yameongeza hatari ya hali ya hewa kavu, ya joto ambao inachangia kuchochea moto wa nyika
Unsplash/Mikhail Serdyukov

COP26 ikifungua pazia WMO yasema miaka 7 iliyopita imevunja rekodi ya joto duniani

Miaka saba iliyopita inaelekea kuwa ya joto zaidi kuwahi kurekodiwa sanjari na kupanda kwa kina cha bahari ni katika viwango vya kuvunja rekodi, kulingana na ripoti ya muda ya shirika la hali ya hewa duniani (WMO) ya hali ya hewa duniani kwa mwaka 2021, iliyotolewa Jleo umapili, wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26, ukifunguliwa Glasgow, Uingereza.

Watu wakiwa katika mto uliofurika Magharibi mwa Haiti baada ya daraja kusombwa na maji kufuatia kimbunga Matthew
MINUSTAH/Logan Abassi

Muda unatutupa mkono kuepuka janga la mabadiliko ya tabianchi:UN Ripoti 

Kupunguzwa kwa muda kwa uzalishaji wa hewa ukaa kulikosababishwa na masharti ya kimataifa ya watu kusalia majumbani wakati wa janga la corona au COVID-19 hakukupunguza kasi ya kuendelea kwa mabadiliko ya tabianchi. Viwango vya gesi chafuzi vimevunja rekodi, na dunia iko njiani  kuelekea hatari joto kali la kupindukia,  imeonya ripoti ya mabadiliko ya tabia nchi iliyotolewa leo na mashirika  mbalimbali. 

22 MACHI 2021

Katika jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Grace Kaneiya anakuletea

-Leo ni siku ya maji duniani na Umoja wa Mataifa umesisitiza kila mtu kutambua thamani ya rasilimali hiyo muhimu ili kuhakikisha watu wote wana fursa ya kuipata kote duniani

-Nchini Sudan Kusini mpango wa Umoja wa Mastaifa UNMISS umeendesha warsha ya siku mbili Yambio na Nzara kwa ushirikiano na serikali ili kuhakikisha vijana, wanawake na jamii wanajikwamua vyema na janga la COVID-19, vita na mabadiliko ya tabianchi

Sauti
12'33"