Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

WIPO

Picha na (NAMS)

Ubunifu wa wanawake wabadili jamii zao #WorldIPDay

Ubunifu wa wanawake katika nyanja mbalimbali kuanzia mavazi, tiba na hata ufugaji sasa unadhihirisha kuwa udadisi wa kundi hilo ukijengewa uwezo, umaskini utasalia historia.

Katika siku ya haki ya ubunifu duniani, Umoja wa Mataifa unaweka bayana utambuzi wake wa mchango wa wanawake katika udadisi wao na ubunifu wa mbinu mbalimbali za kuleta mabadiliko na maendeleo chanya kwenye jamii zao.

Sauti
1'59"

Afrika Kusini yachomoza kwenye usajili wa hataza ugenini

Afrika Kusini imechomoza katika kuwasilisha maombi ugenini ya kusajili hati ya kisheria ili kuepusha kuigwa na watu wengine au hataza.

Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la hakimiliki la Umoja wa Mataifa, WIPO iliyotolewa leo huko Geneva, Uswisi ikiangazia viashiria vya hakimiliki duniani kwa mwaka 2016.

Mkurugenzi Mkuu wa WIPO Francis Gurry amewaambia waandishi wa habari kuwa usajili wa hataza nje ya nchi unaashiria jinsi wabunifu wanavyotaka kueneza teknolojia nje ya mipaka.