Kenya imepiga hatua Afrika katika nafasi ya ubunifu wa kimataifa-WIPO
Shirika la hakimiliki duniani, WIPO leo limezindua ripoti ya maendeleo na ubunifu kimataifa kwa mwaka 2019 huku ikitaja India kama nchi iliyopiga hatua kubwa zaidi kutoka nafasi ya 81 hadi 52 tangu mwaka 2015, pia nchi zingine tatu ambazo zimetajwa kupiga hatua kubwa katika kipindi cha miaka tisa iliyopita ni Kenya, Viet Nam na Maldives.