Botswana: Mkutano wa 73 wa Kamati ya Kanda ya Afrika ya WHO waanza Gaborone
Mkutano wa Sabini na tatu wa Kamati ya Kanda ya Afrika ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO) umeanza hii leo katika mji mkuu wa Botswana, Gaborone huku tukio hilo likishuhudia pia Maabara ya Kitaifa ya Marejeleo ya Virusi vya Ukimwi (VVU) ya Botswana ikipewa hadhi ya kuwa Kituo Kishiriki cha Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni (WHO) cha kufuatilia Ubora.