Skip to main content

Chuja:

wazee

WHO-Europe

Kampeni ya utoaji chanjo ya homa ya mafua makali yaendelea ukanda wa ulaya: WHO

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya ulaya tangu kuanza kwa msimu wa baridi kali katikati ya mwezi Novemba mwaka 2022 wamebaini kuongezeka kwa wagonjwa wanaolazwa kutokana na magonjwa ya homa ya mafua makali au flu,  matatizo ya kupumua na COVID-19. Walio hatarini zaidi kupata maambukizi ya magonjwa hayo ni wahudumu wa afya pamoja na wazee, ndio maana wanaendesha kampeni ya kutoa chanjo. 

Sauti
2'41"
Mwanamke mzee akiwa katika kambi ya wakimbizi wandani nchini Somalia
© UNICEF/Sebastian Rich

WHO yatoa vipaumbele 5 kukabiliana na unyanyasaji wa wazee

Leo ni siku ya kuhamasisha kupinga unyanyasaji dhidi ya wazee na katika kuadhimisha siku hii Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO na wadau wake wamechapisha vipaumbele vitano vitakavyosaidia kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji wa wazee na hivyo kuchangia katika kuboresha afya, utawi na utu wao.

Wazee wawili wakiwa wameka katika benchi.
Photo: World Bank/Celine Ferre

Janga la COVID-19 limeongeza ukatili dhidi ya wazee: mtaalam wa UN aonya

Wakati mitazamo ya zamani kuhusu uzee tayari inadhoofisha uhuru wa wazee katika kufanya uchaguzi na maamuzi yao wenyewe, janga la COVID-19 limeleta zahma zaidi, dhuluma na kutelekezwa dhidi watu hao, ameonya leo mtaalam huru wa  haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, katika ujumbe wake kuhusu Ulimwengu siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhudu ukatili dhidi ya wazee.