Waogiek tunajikongoja Kenya,serikali tushikeni mkono: Prengei
Wakati jukwaa la kimataifa la watu wa asili likiwa katika wiki ya pili kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, watu wa asili kutoka jamii ya Ogiek nchini Kenya wanasema wanakimbiza treni ya SDGs lakini bila mkono wa serikali kuikamata itakuwa mtihani.
Watu Asili kushiriki na kushirikishwa katika utunzaji wa mazingira na viumbe hai: Burundi
Kongamano la watu asili kutoka eneo la Maziwa makuu barani Afrika limehitimishwa mjini Bujumbura Burundi . Lilijikita katika jinsi Jamii hiyo wanavyoweza kushiriki na kushirikishwa katika utunzaji wa mazingira na viumbe hai katika maeneo wanakoishi.
Jamii hiyo imekuwa inanyooshewa kidole kwa kuhusika na sehemu kubwa katika uharibifu wa mazingira, madai ambayo wanayakana wakitaja kwamba mazingira ni sehemu ya maisha yao.
Kutoka bujumbura , Muandishi wetu wa Maziwa Makuu Ramadhani KIBUGA amefuatilia kongamano hilo na kuandaa makala hii.