Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

wasaka hifadhi

Moja ya mitaa ya mji mkuu wa Rwanda, Kigali
UN/Rick Bajornas

Tunazifuatilia taarifa kuwa Uingereza inataka kuwahamishia nchini Rwanda wasaka hifadhi  

Kufuatia uwepo wa taarifa za kuwa Uingereza imeingia makubaliano na Rwanda ya kuwahamisha wasaka hifadhi nchini Uingereza na kuwapeleka Rwanda, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema linaelewa kuwa serikali ya Uingereza inatangaza ushirikiano wa uhamiaji na maendeleo ya kiuchumi na nchi ya Rwanda lakini linahitaji kuyaona makubaliano hayo kwanza kabla ya kutoa maoni.

Sauti
1'21"
Wahamiaji wakisajiliwa katika Kituo cha Usafiri cha Agadez nchini Niger.
IOM

Niger yapongezwa kwa ukarimu kwa wasaka hifadhi na wakimbizi

Viongozi wa mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la Kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi na lile la Uhamiaji IOM Antonio Vittorino wamefanya ziara nchini Niger, huko Agadez ambalo ni eneo la mpito la watu wanaotafuta hifadhi na wahamiaji nchini Niger ambalo limeongezeka kuwa na idadai kubwa ya watu wenye kuhitaji msaada wa usalama na fursa. 

Sauti
2'52"
Tanzania
World Bank/Hendri Lombard

Tanzania yawaweka kizuizini wasaka hifadhi, UNHCR yatafuta njia ya kufikia suluhu.  

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, kupitia taarifa yake iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi, limesema linasikitishwa sana na msururu wa ujumbe wa kusikitisha ambao limekuwa likipokea kutoka kwa kikundi cha waomba hifadhi 10 ambao hivi sasa wamewekwa kizuizini katika eneo la Mutukula, kaskazini magharibi mwa Tanzania.