Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanyamapori

20 FEBRUARI 2024

Karibu kusikiliza jarida la habari za Umoja wa Mataifa hii leo ikiwa ni Siku ya Kimataifa ya Haki ya Kijamii Duniani. 

Jarida linaletwa kwako na LEAH MUSHI na kubwa hii leo ni mada kwa kina kutoka nchini Kenya ambako serikali na wadau wa wanyamapori wamechukua hatua kulinda moja ya Wanyama walio hatarini kutoweka , Faru. 

Pia utapata fursa ya kusikiliza muhtasari wa habari na ujumbe kutoka mashinani. 

Karibu. 

Sauti
13'11"
Tembo wa Afrika wameorodheshwa kuwa hatarini na Muungano wa Kimataifa wa Uhifadhi wa Mazingira (IUCN), huku wanyama hao wakiwindwa kwa ajili ya pembe zao za ndovu.
UNEP GRID Arendal/Peter Prokosch

UNODC imesaidia KWS kupambana na ufisadi ili kulinda wanyamapori Kenya

John Mugendi, Mkurugenzi Msaidizi Mwandamizi wa Shirika la Huduma ya Wanyamapori la Kenya, leo jijini Nairobi Kenya, akitambua usaidizi kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) amesema, "Kuhifadhi hazina ya wanyama pori Kenya yenye thamani kubwa si chaguo tu bali ni wajibu wa vizazi vijavyo." 

UNDP/Sawiche Wamunza

Matunda ya ubia katika kuhifadhi wanyamapori wazaa matunda pori la Waga Tanzania

Nchini Tanzania kumulika ni kwa vipi mradi wa Jumuiya za Hifadhi za WAnyamapori, WMAs, unaotekelezwa kwa pamoja kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii nchini humo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP wa kuzuia ujangili na uhifadhi wa wanyamapori umesaidia jamii kunufaika sio tu na uwepo wa wanyamapori kwenye maeneo yao lakini pia kuishi kwa utangamano na wanyama kwa kuzingatia kuwa leo ni siku ya wanyamapori duniani na ujumbe ni ushirikishaji jamii katika hifadhi ya wanyamapori.

Sauti
5'35"

02 MACHI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia mada kwa kina na ninakupeleka nchini Zimbabwe kumulika harakati za uhifadhi wa wanyamapori, ikiwa ni kuelekea siku ya wanyamapori duniani hapo kesho. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo UNICEF, WHO na UNECE. Na leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, je wajua maana ya msemo "KAUKA NIKUVAE SANDUKU MSUMARI"? Baki nasi!

Sauti
11'43"

27 Desemba 2022

Hii leo katika jarida la Umoja wa Mataifa utasikia mada kwa kina kuhusu utalii endelevu nakulinda wanyamapori walio hatarini kutoweka nchini Tanzania.

pia utasikia habari kwa ufupi kuhusu marufuku ya wanawake nchini Afghanistan kufanya kazi kwenye NGOs, Wakimbizi waliokwama baharini kwa mwezi mzima waokolewa na Indonesia na Wakimbizi wa ndani nchini Ukraine wapatiwa msaada katika msimu huu wa baridi. 

Na tukiwa bado kwenye msimu wa sikukuu, wakimbizi kutoka nchini Ukriane wanajaribu kufanya kila jitihada kuhakikisha nao wanasherehekea sikukuu hizi.

Sauti
13'5"