Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali mauaji ya waandamanaji huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akisema kitendo hicho hakikubaliki.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC watu sita wameuawa jumapili kwenye mji mkuu Kinshasa wakati wa maandamano yaliyoandaliwa na kanisa katoliki nchini humo. John Kibego na ripoti kamili.