Chuja:

wanawake na biashara

Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi Tanzania
UN News

FAO Tanzania yazindua tawi la Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA

Katika kutekeleza lengo namba 8 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuhusu ajira za staha na ukuaji kiuchumi sambamba na namba 5 la usawa wa kijinsia, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo duniani FAO nchini Tanzania,  limezindua tawi la tatu la Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA kupitia mradi wake wa kukuza mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi katika ziwa Tanganyika.

Sauti
4'19"
UNICEF/Shehzad Noorani

Mradi wa UNIDO umeniondolea Umasikini

Mradi wa kuwezesha wanawake nchini Sudan Kusini unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la maendeleo ya viwanda UNIDO kwa ufadhili wa serikali ya Canada umekuwa mkombozi mkubwa hasa kwa wanawake wavuvi na wakulima nchini mjini Juba nchini humo sio tu kwa kuwawesha kulisha familia zao lakini pia kupambana na umasikini.

John Kibego anafafanua zaidi