Skip to main content

Chuja:

wanamgambo

Machafuko Tanganyika na Kivu Kusini DRC, yawaweka watoto njia panda: UNICEF

Watu zaidi ya millioni moja , wakiwemo watoto 800,000 wamesambaratishwa  na ghasia za kikabila pamoja na mapigano kati ya vikosi vya serikali,dhidi ya makundi  yenye silaha na makundi ya wanamgambo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo yaani DRC.

Hii ni kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalowashughulikia watoto UNICEF, ambalo linasema  vurugu hizo nyingi ziko katika mikoa ya Kivu Kusini na Tanganyika. UNICEF limekariri kuwa kwa sasa idadi kubwa ya watu dunaini waliokimbia makazi yao kutokana na ghasia inapatikana nchini DRC ambako inafikia watu millioni 1.3.