Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

wakimbizi wa Rohingya

24 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na Mwanaisha Ulenge ni Mwanamke Mwanasayansi Mhandisi, Mbunge nchini Tanzania vilevile Mjumbe wa Shirikisho la Mabunge Duniani (IPU) na hivi karibuni akiwa katika ziara ya kikazi hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa Anold Kayanda alipata fursa ya kujadiliana naye kuhusu nafasi ya mwanamke katika sayansi na teknolojia.

Sauti
11'24"

Jarida 18 Agosti 2021

Katika jarida hii leo utasikia kuhusu uzinduzi wa mkakati wa Mabadiliko ya Kidigitali ya Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa. Pia utasikia wakimbizi wa ndani nchini Somalia wanavyoteseka na njaa pamoja na utoaji chanjo kwa wakimbizi wa Rohingya huko kambini Coxs Bazar.

katika makala leo tunaangazia utunzaji wa mazingira kwa vijana nchini Rwanda. 

Sauti
13'7"
©WHO/Blink Media/Fabeha Monir

wakimbizi wa Rohingya nchini Bangladesh wapatiwa chanjo ya CORONA

Maelfu ya wakimbizi wa Rohingya kwenye kambi ya Cox’s Bazar nchini Bangladesh sasa wameanza kupokea chanjo dhidi ya COVID-19 kama sehemu ya mkakati mkubwa wa kitaifa wa kudhibiti kusambaa kwa virusi vya gonjwa hilo.

(TAARIFA YA LUCY IGOGO) 
Katika kituo cha afya cha kwenye makazi ya Cox’s Bazar wakimbizi wameketi katika foleni wakisubiri kuitwa na kupewa maelezo na daktari kabla ya kupata chanjo dhidi ya corona. 

Sauti
2'9"

WHO kuanza kampeni ya chanjo dhidi ya dondakoo kwa wakimbizi wa Rohingya

Shirika la afya ulimwenguni WHO leo llimetangaza kuzindua kampeni kubwa ya chanjo ili kusitisha kusambaa kwa maradhi ya kupumua miongoni mwa wakimbizi wa Rohigya walioko Cox Bazar nchini Bangladesh.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva hii leo Fadela Chaib msemaji wa WHO amesema hadi kufikia siku mbili zilizopita kuna wakimbizi sita waliofariki dunia kutokana na ugonjwa wa dondakoo na visa zaidi ya 110 vilivyoambukizwa ugonjwa huo.