Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

wajasiriamali

02 MEI 2023

Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina na leo tunamulika juhudi za kumkwamua mjasiriamali hasa nchini Kenya. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo ziara za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Qatar, haki za binadamu na misaada kutoka mashirika nchini Sudan. Katika mashinani na kuelekea siku ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari hapo kesho, tunakuletea ujumbe wa Mwandishi wa Habari kutoka Uingereza kuhusu changamoto zinazowakumba waandishi wa habari.

Sauti
12'24"
Susan Auma Mang’eni katibu mkuu idara ya ukuzaji wa biashara ndogondogo iliyo ndani ya wizara mpya ya ushirika na ukuzaji wa biashara ndogondogo au ujasiriamali  akihojiwa na Flora Nducha wa Idha ya Kiswahili ya UM jijini New York.
UN News/Anold Kayanda

Ni wakati wa nchi zinazoendelea kujipanga jinsi ya kujitegemea kiuchumi: Susan Auma

Changamoto mbalimbali zinazoendelea duniani ikiwemo athari zilizoletwa na janga la COVID-19 katika mnyororo mzima wa usambazaji wa bidhaa duniani, katika ukuaji wa uchumi, vita inayoendelea nchini Ukraine na majanga ya asili kama ukame vimechangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma jitihada za ufadhili wa maendeleo duniani kote na nchi nyingi hasa zinazoendelea zimejikuta katika wakati mgumu.

22 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida leo tunajikita katika mada kwa kina kuangazia harakati za kusongesha viwanda vidogo vidogo barani Afrika hususan nchini Tanzania, kwa kuzingatia kuwa mwishoni mwa wiki ilikuwa ni siku ya viwanda barani Afrika.

Pia utapata fursa ya kusikiliza habari kwa ufupi

Sauti
11'41"
Picha: UNFPA/Omar Gharzeddine

Mtaala wa ujasiriamali wawezesha wanafunzi Msumbiji kujikimu

Barani Afrika idadi ya vijana kama ilivyo katika mabara mengine inaongezeka kila uchao. Kasi ya ongezeko hilo haiendi sambamba na mabadiliko ya stadi shuleni ili waweze kupata ujuzi wa kuwawezesha kukabiliana na maisha yao. Ni kwa kuzingatia hilo, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la maendeleo ya viwanda, UNIDO limeanzisha mradi wa kujumuisha mtaala wa ujasiriamali katika shule za msingi na sekondari barani Afrika.

Sauti
3'30"
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Kina mama wajasiriamali waneemeka na mafuta Uganda

Upatikanaji wa bidhaa ya mafuta nchini Uganda umeleta faraja kwa mamilioni ya wananchi ambao sasa wanaona nuru ya kupungua kwa bei ya bidhaa hiyo katika siku za usoni. Na neema hiyo sio kwa waendesha magari tu bali pia kwa wafanya biashara ndogondogo au wajasiriamali wakiwemo wanawake. Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego amewatembelea baadhi ya wanawake walioanza kunufaika na uwepo wa shughuli za uchimbaji mafuta katika eneo la ziwa Albert nchini humo ili  kupata ufafanuzi zaidi unagana naye