Wajasiriamali wanawake kwenye mizozo wanahitaji usaidizi wa kimkakati na si misaada
Suala la kuwekeza kwa wanawake wajasiriamali kwenye maeneo yenye mizozo duniani limepatiwa uzito hii leo mwishoni mwa mkutano wa 5 wa Umoja wa Mataifa kuhusu uwekezaji kwa wajasiriamali, WEIF 2024 huko Manama, mji mkuu wa Bahrain, jukwaa lililoratibiwa na Umoja wa Mataifa na wadau wake.