Kitendo cha kushindwa kuwafikia watoto wa kabila la Rohingya ambao bado wamesalia nchini Myanmar kinatutia shaka kubwa kwa kuwa wanaishi kwenye mazingira ya kusitikisha.
Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF hii leo kufuatia ziara ya msemaji wake huko jimbo la Rakhine nchini Myanmar hivi karibuni.
Marixie Mercado amesema watoto wapatao 60,000 wamenasa kwenye kambi dhalili katikati mwa jimbo hilo la Rakhine wakiwa katika hali mbaya huku ulimwengu ukielekeza zaidi usaidizi wake kwa wakimbizi 655,000 ambao wameingia Bangladesh.