Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Wahudumu wa kibinadamu

19 AGOSTI 2025

Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika umuhimu wa wahisani. Pia tunaangazia siku ya Wahudumu wa Kibinadamu Duniani tukikuletea ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaomulika haki zao, na hali ya usalama nchini DRC.

Sauti
10'41"
UNICEF

Gaza ni tishio lililo kimya - Dkt. Younis

Umoja wa Mataifa umetenga siku maalum ya kuwashukuru watoa huduma za misaada ya kibinadamu na siku hiyo ni Agosti 19 kila mwaka. Takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu zinaeleza kuwa mwaka huu wa 2025, watu milioni 305.1 kutoka nchi 72 wanahitaji usaidizi wa kibinadamu ambao utagharibu dola bilioni 47.4. Takwimu hizi zinaonesha umuhimu na uhitaji wa watoa huduma wa kibinadamu.

Sauti
3'12"

18 AGOSTI 2025

Jaridani leo tunaangazia amani na usalama nchini Ukraine, na ajira kwa vijana katika sekta ya biashara ya kilimo vijijini. Makala tunaangaazia wahudumu wa kibinadamu Gaza, na mashinani tunamulika afya kwa wanawake wajawazito nchini Tanzani.

Sauti
9'57"

20 AGOSTI 2024

Karibu kusikiliza jarida linalo letwa kwako na Anold Kayanda ambapo hii leo anakuletea mada kwa kina ambayo inamulika wahudumu wa kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan kile kinachosababisha waendelee kutekeleza jukumu hilo licha ya changamoto za kiusalama wanazopitia. 

Pia utasikia muhtasari wa habari ukiletwa kwako na Leah Mushi ambapo ameangazia suala la nishati ya mafuta huko Gaza, ugonjwa wa Mpox huko barani ulaya, na maadhimisho ya siku ya mbu duniani yanayolenga kuelimisha jamii jinsi ya kupambana na mdudu huyo hatari. 

Sauti
9'56"

19 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha

-Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibindamu na masula ya dharura OCHA yatoa shukrani zake kwa wahudumu wa kibinadamu kokote waliko katika kuokoa maisha.

- Ikiwa leo ni siku ya huduma za kibinadamu duniani Umoja wa Mataifa umesema unawaenzi wahudumu hao ambao wanakabiliana na changamoto lukuki katika kuokoa na kuboresha maisha ya mamilioni ya watu.

Sauti
13'27"