Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Wahudumu wa afya

Muuguzi akitoa chanjo ya Polio kwa mtoto mchanga katika hospitali nchini Malawi
© UNICEF/Giacomo Pirozzi

Mwongozo mpya wa WHO/ILO kuwalinda wahudumu wa afya

Taarifa ya pamoja iliyotolewa leo na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na lile la kazi duniani ILO imetoa mwongozo mpya kuhusu kuendeleza na kutekeleza mipango imara ya afya na usalama kazini kwa wafanyakazi wa sekta ya afya, wakati huu janga la COVID-19 likiendelea kuwapa shinikizo kubwa wafanyakazi hao.  

Muhudumu wa afya akimuhudumia mgonjwa katika ukumbi uliobadilishwa matumizi na kuwa wodi ya muda ya wagonjwa wa COVID-19 huko New Delhi, India
© UNICEF/Amarjeet Singh

WHO yatoa wito wa watoa hudumu ya afya kulindwa dhidi ya COVID-19

wafanyikazi wa huduma za afya kwa jumla wamelipa gharama kubwa wakati wa janga la COVID-19. Na shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani (WHO) na washirika wake leo mjini Geneva Uswis wamezindua ombi la dharura la kuchukua hatua madhubuti ili kulinda vyema afya na wahudumu wa afya kote ulimwenguni dhidi ya virusi vya Corona na changamoto zingine za kiafya.

UNSOM

Usalama wa wahudumu wa afya ni msingi wa usalama wa wagonjwa 

Ikiwa leo ni siku ya usalama wa wagonjwa duniani, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO limesema hakuna taifa linaweza kuwaweka salama wagonjwa wake iwapo linapuuza usalama wa wahudumu wa afya hasa wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 ambalo bado linatikisa maeneo mengi duniani. John Kibego na taarifa kamili. 

Kutana na Souleymane Hamani Zada, mhudumu wa afya katika kituo cha afya cha Guidan Roumdji nchini Niger. Katika zama hizo za COVID-19 anahakikisha amevalia mavazi mahsusi kujikinga yeye na wale anaowahudumia. 

Sauti
2'29"
Wakiwa ewamevalia mavazi ya kujikinga, daktari mwanamke anayeongoza kundi la wataalamu wa afya wanaojitolea kuhudumia wagonjwa wa COVID-19 na wanaochunguzwa katika hospitali ya jamii Ufilipino.
UN Women/Louie Pacardo

WHO yazindua katiba ya usalama wa wahudumu wa afya 

Ikiwa leo ni siku ya usalama wa wagonjwa duniani, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO limeangazia wahudumu wa afya na wagonjwa wanaowahudumia hasa wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 ambalo bado linatikisa maeneo mengi duniani. 

Sauti
2'29"