Watu waliokufa kwa COVID-19 mwaka 2022 wafikia milioni 1: WHO
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema watu hawapaswi kujisahau wala kuchukulia kama janga la COVID-19 limeisha duniani kwani bado lipo na linaendelea kuuawa mamilioni ya watu.