Skip to main content

Chuja:

Wafanyakazi wahamiaji

© ILO

Wahamiaji wa kimataifa waongezeka kutoka Milioni 164 mpaka 169

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shjirika la kazi duniani ILO inakadiria kwamba kati ya mwaka 2017 na 2019 idadi ya wahamiaji wa kimataifa imeongezeka kutoka milioni 164 hadi milioni 169, sanjari na kuongeza idadi ya wafanyakazi wahamiaji. 

Kwa mujibu wa ripoti hiyo “Makadirio ya kimataifa ya ILO kuhusu wafanyakazi wahamiaji:matokeo na mfumo” inaonyesha kwamba mwaka 2019 wanayakazi wahamiaji wa kimataifa walikuwa karibu asilimia 5 wa wafanyakazi wote duniani na kuwafanya kuwa chachu muhimu ya uchumi wa dunia. 

Sauti
2'50"

Juni 30 2021

Katika Jarida hii leo utasikia huko Paris nchini Ufaransa kumeanza jukwaa la siku tatu la kusaka kusongesha usawa wa kijinsia kwa kujumuisha vijana katika kufanikisha lengo hilo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ya Umoja wa Mataifa. Mkutano huo unafanyika kwa kuzingatia kuwa miaka 25 baada ya mkutano wa kimataifa wa wanawake huko Beijing nchini China, bado usawa wa jinsia unasalia ndoto kwa maeneo mengi.

Sauti
13'54"