UN yawaenzi wafanyakazi wake waliopoteza maisha kazini
Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliopoteza Maisha wakiwa kazini leo wameenziwa kwenye hafla maalum kwenye Umoja wa Mataifa kwa ushujaa wao na kwa huduma yao chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuokoa vizazi vijavyo.