Mwongozo mpya wa WHO/ILO kuwalinda wahudumu wa afya
Taarifa ya pamoja iliyotolewa leo na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na lile la kazi duniani ILO imetoa mwongozo mpya kuhusu kuendeleza na kutekeleza mipango imara ya afya na usalama kazini kwa wafanyakazi wa sekta ya afya, wakati huu janga la COVID-19 likiendelea kuwapa shinikizo kubwa wafanyakazi hao.