Chuja:

wafanyakazi

Muuguzi akitoa chanjo ya Polio kwa mtoto mchanga katika hospitali nchini Malawi
© UNICEF/Giacomo Pirozzi

Mwongozo mpya wa WHO/ILO kuwalinda wahudumu wa afya

Taarifa ya pamoja iliyotolewa leo na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na lile la kazi duniani ILO imetoa mwongozo mpya kuhusu kuendeleza na kutekeleza mipango imara ya afya na usalama kazini kwa wafanyakazi wa sekta ya afya, wakati huu janga la COVID-19 likiendelea kuwapa shinikizo kubwa wafanyakazi hao.  

31 DESEMBA 2020

Katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Anold Kayanda anakuletea salamu za mwisho wa mwaka kutoka kwa wafanyakazi

-Wanazungumzia mambo mbalimbali ikiwemo malengo ya maendeleo endelevu SDGs

-Je mwaka 2020 umekuwaje?

-Nini changamoto kubwa iliyokabili kazi zao kwa mwaka 2020

-Mashinani washirika wetu na maripota wetu wanasemaje?

-Na nini msikilizaji, mtazamaji, na mfuatiliaji wa vipindi vya Umoja wa Mataifa atarajie mwaka 2021

 

Sauti
9'57"
Wanawake katika jimbo la Copperbelt nchini Zam,bia wanaofanya kazi katika mfumo wa kilimo bora wanaongeza uzalishaji wa mbogamboga wanaouza katika masoko ya wenyeji( kutoka maktaba 2015)
ILO/Marcel Crozet

Usalama na afya kazini ni haki ya kila mtu:ILO

Katika kuadhimisha miaka 100 ya shirika la kazi ulimwenguni ILO ambalo dhamira yake ni kuhakikisha ajira bora na zenye hadhi kwa kila mtu, leo ikiwa ni siku ya usalama na afya kazini limetoa wito kwa serikali, waajiri na wafanyakazi kushiriki katika kujenga mazingira salama na yenye afya kazini.

UN yapunguza bajeti yake

Bajeti ya umoja wa Mataifa kwa mwaka 2018-2019 yenye kurasa zaidi ya elfu 8 zilizosheheni maelezo ya mipango mbalimbali na takwimu za taasisi hii kubwa zaidi duniani ilipitishwa mwishoni mwa juma na nchi 193 wanachama wa Umoja huo ikiwa na upungufu wa mamilioni ya dola ikilinganishwa na mwaka 2016-2017 unaomalizika. Tuungane na Assumpta Massoi anayetudadavulia zaidi kuhusu kilichomo, kilichoathirika zaidi na matarajio ya baadaye katika kuhakikisha Umoja wa Mataifa unafanya kazi kwa ufanisi na unawajibika kwa nchi wanachama na walipa kodi.