Vifo vya waafrika 23 katika mpaka wa Melilla wataalamu wa UN wataka uwajibikaji
Wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa hii leo wameyataka mataifa ya Morocco na Hispania kuhakikisha uchunguzi huru unafanyika na hatua kuchukuliwa kwa wale waliohusika na vifo vya waafrika 23 waliokuwa wakijaribu kuvuka mpaka wa Melilla unaotenganisha nchi hizo mbili wakitaka kwenda ulaya.