Ripoti ya UN kuhusu masuala ya haki za fidia kwa Waafrika na wenye asili ya Kiafrika
Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa, Septemba 03, imetoa ripoti ikizitaka nchi wanachama na wadau wengine kuongeza juhudi katika kuhakikisha upatikanaji wa haki za fidia kwa Waafrika na watu wenye asili ya Kiafrika. Hii ni pamoja na msamaha wa dhati, kutafuta ukweli, kuenzi kumbukumbu, kutoa msaada wa kiafya na kisaikolojia pamoja na fidia ya kifedha.