Vyeti vya kuzaliwa

29 AGOSTI 2022

Flora Nducha anakuletea jarida lililo sheheni habari mbalimbali kuanzia nchini Ethiopia ambapo tume ya Kimataifa ya wataalamu wa Haki za binadamu nchini Ethiopia imekasirishwa na kuzuka upya kwa uhasama kati ya serikali ya Ethiopia na chama cha Tigray People's Liberation Front tangu wiki iliyopita na kuzitaka pande zote mbili kurudi kwenye meza ya mazungumzo kwani wanaoteseka ni raia.

Wakimbizi wa Burundi wakioko katika kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma nchini Tanzania wameshukuru kwa watoto wao kupatiwa vyeti vya kuzaliwa 

Sauti
10'26"
ADB/Al Benavente

UNHCR yasaidia wanajamii wa Sama Bajau kupata vyeti vyakuzaliwa

Cheti cha kuzaliwa ni moja ya nyaraka muhimu kwa utambulisho wa mtu, lakini pia kigezo cha kusaidia kupata huduma za msingi kama za afya, elimu na hata hifadhi ya jamii.

Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR mambo ni tofauti sana kwa jamii ya wavuvi ya Sama Bajau inayoishi kwenye mwambao wa Ufilipino, Malaysia na Indonesia ambao kwa miaka mingi wamekosa huduma kwa kutokuwa na vyetu vya kuzaliwa na hivyo kukosa utaifa.

Sauti
2'29"