Chuja:

Volker Turk

Watoto wanasubiri kupokea chakula cha lishe bora katika klinki moja huko jiji la Nampo, DPRK
© UNICEF/Olga Basurmanova

Korea Kaskazini semeni ukweli na mtende haki kwa watu waliotoweshwa na kutekwa nyara: Türk

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za binadamu Volker Türk hii leo jijini Geneva nchini Uswisi ametoa ripoti ya kina inayoonesha mateso yanayoendelea ya waathirika wa kutoweshwa na kutekwa nyara nchini Korea Kaskazini na kutaka wale wote wanaohusika wachukuliwe hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani ndani ya nchi au mahakama za kimataifa.

Geti la kuingia kwenye makao makuu ya ofisi ya haki za binadamu OHCHR mjini Geneva Uswis
UN Photo/Jean-Marc Ferré

Uchunguzi huru na wa haki lazima ufanyike dhidi ya waliokufa Laas Canood: Turk

Kutoka Geneva nchini Uswisi Kamisha Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa , Volker Turk ametoa wito kwa mamlaka ya Somalia kuhakikisha uchunguzi huru unafanyika bila upendeleo kufuatia mauaji yaliyotokea baada ya mapigano makali kuanzia tarehe 5 mwezi huu wa Februari nchini humo kati ya vikosi vya usalama na wanajamii wa ukoo wa Laas Canood.

EQUIS Justicia para las mujeres/Scopio

Waliofungwa kwa kusimamia haki zao waachiliwe huru- Türk

Kufuatia kuanza kwa maadhimisho ya miaka 75 tangu kupitishwa kwa Tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, UDHR, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu, Volker Türk ametoa wito kwa serikali duniani kote na mamlaka zote zinazoshikilia watuhumiwa kuwapatia msamaha au kuwaachilia huru wale wote walioswekwa ndani kwa kutekeleza haki zao za msingi.

Sauti
1'55"
Mtoto akiwa amesimama karibu na pampu ya maji iliyozingirwa na maji ya mafuriko huko Gatumba nchini Burundi.
© UNICEF/Karel Prinsloo

Haki za binadamu ni moyo wa juhudi za kukabiliana athari za tabianchi: Türk

Kuelekea mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa Tabianchi, COP27 huko Sharm el-Sheikh nchini Misri, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu Volker Türk amesema anatarajia matokeo ya mkutano huyo yatazingatia haki ya kila mtu ya kuishi ambaypo kwa sasa ipo hatarini kutokana na uwepo wa hatua zisizotosheleza za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

UN Kenya/Newton Kanhema

UN yapongeza Kenya kwa kutumia sheria ya kimataifa kushtaki watuhumiwa wa uhalifu baada ya uchaguzi mkuu 2017

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameipongeza serikali ya Kenya kwa kile alichoeleza ni hatua muhimu ya kuelekea uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Kenya, kufuatia uamuzi wake wa wa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa kuwafungulia mashitaka maafisa wakuu wa polisi kwa mauaji, ubakaji na utesaji kama uhalifu dhidi ya ubinadamu kufuatia vurugu zilizotokea wakati wa uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo mwaka 2017. Leah Mushi anataarifa zaidi.

Sauti
1'59"
Mji mkuu wa Nairobi, Kenya
World Bank/Sambrian Mbaabu

Heko Kenya kwa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa- UN

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameipongeza serikali ya Kenya kwa kile alichoeleza ni hatua muhimu ya kuelekea uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Kenya, kufuatia uamuzi wake wa wa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa kuwafungulia mashitaka maafisa wakuu wa polisi kwa mauaji, ubakaji na utesaji kama uhalifu dhidi ya ubinadamu kufuatia vurugu zilizotokea wakati wa uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo mwaka 2017

Sauti
1'59"