UNICEF na serikali ya Japan kuwanusuru walioathirika na Tsunami na volcano Tonga
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na serikali ya Japani wametangaza ushirikiano mpya wa kuchangia dola milioni 1.25 kuisaidia serikali ya Ufalme wa Tonga kuhakikisha kuwa takriban watu 19,250 wakiwemo watoto 10,000 walioathiriwa na mlipuko wa volcano na tsunami hivi karibuni wanapata maji safi ya kutosha ya kunywa, mazingira safi , pamoja na afya njema.