Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

VNRs

10 JULAI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu na walinda amani nchini DRC. Makala tuankupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Chad, kulikoni?   

Sauti
11'17"
UN/Steven Bornholtz

UN: Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa HLPF kuhusu SDG’s limengoa nanga leo

Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu ,malengo ya maendeleo endelevu lijulikanalo kama HLPF limeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa hapa New York Marekani chini ya mwamvuli wa baraza la kiuchumi na kijamii ECOSOC.

Jukwaa hilo ambalo litakunja jamvi 20 Julai mwaka huu limebeba maudhui "Kuharakisha kujikwamua kutokana na janga la ugonjwa wa  virusi vya corona au COVID-19 na utekelezaji kamili wa ajenda ya 2030 ya maendeleo endelevu katika ngazi zote".

Sauti
2'38"