Mbinu mpya za pamoja zitawezesha kukabili kitisho cha ugaidi
Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na ugaidi, Vladimir Voronkov, amesema suala ya kwamba ugaidi unaendelea kuwa tishio la amani na usalama duniani linahitaji siyo tu kufuatiliwa na Baraza la Usalama bali pia mbinu mpya za pamoja kama iliyoelezwa na Katibu Mkuu Antonio Guterres kwenye Ajenda yake ya Pamoja.