Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Vladimir Voronkov

Sinjar nchini Iraqi Kurdistan ilivamiwa na wapiganaji wa ISIL wakati kundi lenyewe la kigaidi lilidhibiti mji.
UN OCHA/GILES CLARKE

ISIL bado ni kitovu cha tishio la ugaidi :UN

Licha ya kupoteza udhibiti wa moja ya maeneo ya mwisho waliyokuwa wakiyahidhi nchini Iraq na kuuawa kwa kiongozi wake, kundi la kigaidi la ISIL linasalia kuwa kitovu cha tishio la ugaidi kimataifa amesema afisa wa Umoja wa Mataifa kwenye Baraza la usalama hii leo Ijumaa.

Baraza la Usalama wakati wa kikao cha kujadili tihsio dhidi ya usalama kimataifa unaosababishwa na vitendo vya kigaidi uliofanyika Machi 28, 2019, New York.
UN Photo/Eskinder Debebe)

Baraza la Usalama lapitisha azimio la aina yake la kupinga ufadhili wa ugaidi

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio la aina yake ambalo linazuia ufadhili wa vikundi vya kigaidi kote ulimwenguni.

Akihutubia baraza hilo kwa njia ya video kutoka Roma, Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na masuala ya ugaidi, Vladmir Voronkov amesema kupitishwa kwa azimio hilo kumefanyika wakati muafaka, wakati huu ambapo mashambulizi ya hivi majuzi yameonyesha kwamba makundi ya kigaidi yana raslimali halali na zisizo halali za kupata fedha.

Wapiganaji mamluki wanaelekea Libya na Yemen- Voronkov

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na kikao kujadili wapiganaji mamluki wanaojiunga na vikundi vya kigaidi, jambo ambalo linatishia amani na usalama duniani.

Akihutubia kikao hicho, mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabili ugaidi Vladimir Voronkov amesema suala la wapiganaji mamluki kutumikia vikundi vya kigaidi ni jambo gumu na linalobadilika kila uchao.

Amewapatia wajumbe takwimu zinazoonyesha makadirio kwamba wapiganaji zaidi ya elfu 40 kutoka zaidi ya mataifa 110 wamejiunga na vikundi vya kigaidi vinavyopigana huko Syria na Iraq.