Chuja:

virusi

Homa ya nguruwe ambayo inaambukiza sana na inaweza kuwa na athari kubwa kwa wafugaji wadogo. (Maktaba Machi 2017)
IAEA/Laura Gil Martinez

Virusi visivyojulikana vipatavyo 850,000 viko kwa wanyama na ndege na vinaweza kuathiri binadamu :IPBES/CBD Ripoti

Ripoti mpya iliyotolewa leo na jukwaa la kimataifa la sera za kisayansi kuhusu bayoanuai na huduma za mifumo ya viumbe (IPBES) na kutathiminiwa na mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya bayoanuai (CBD), imeonya kwamba majanga makubwa ya milipuko ya magonjwa yako njiani laki hatua madhubuti zikichukuliwa hatari inaweza kupunguzwa.

Sauti
5'57"
National Institute of Allergy and Infectious Diseases, NIH, US

Kenya kuhakikisha kuna miakakati endapo Virusi vya Corona vitazuka:WHO

Shirika la afya ulimwenguni WHO jana Alhamisi limetangaza kuwa virusi vipya vya corona ni dharura ya afya ya kimataifa inayotia wasiwasi likizitaka nchi zote kuchukua tahadhari na kujiandaa endapo virusi hivyo vitazuka katika nchi zao. Kwa sasa virusi hivyo kitovu chake kimekuwa mji wa Wuhan nchini China ambako Kwa mujibu wa WHO jumla ya visa 9692 vimethibitishwa katika majimbo 31, na kati ya hivyo watu 1239 wako katika hali mbaya, 213 wamefariki dunia na wagonjwa 103 wametibiwa, kupona na kuruhusiwa kwenda nyumbani. Na nje ya China kuna visa 68 vilivyothibitishwa katika nchi 18.

Sauti
5'41"