Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Vanessa Nakate

Mtoto mwenye umri wa miaka 11 akijipatia ahueni ya joto kali kwa kucheza kwenye chemchem ya maji huko  Uzbekhstan
UNICEF/Pirozzi

Watoto milioni 559 duniani kote wanataabika na joto kali kwa sasa, idadi itaongeza na kufikia zaidi ya bilioni 2 mwaka 2050.

Kuelekea mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP27utakaofanyika nchini Misri barani Afrika, shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto UNICEF wametoa ripoti ya kuonesha athari za mabadiliko ya tabianchi kwa watoto katika kipindi cha kuanzia sasa mpaka mwaka 2050.

© UNICEF/Translieu/Nyaberi

Nitatumia ubalozi mwema kupaza sauti kwa maslahi ya watoto - Vanessa

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF leo limemteua na kumtangaza mwanaharakati wa mazingira kutoka nchini Uganda Vanessa Nakate kuwa balozi mwema mpya wa shirika hilo. 

Vanessa Nakate, Balozi mwema wa UNICEF, akiwa ziarani Turkana nchini Kenya alitembelea hospitali ya rufaa ya Lodwar na hapo anazungumza na mtoto Eunice Asukuku ambaye alifikishwa hospitali kwa tatizo la utapiamlo mkali, kuvimba mwili na ukosefu wa damu. Chanzo cha matatizo ni uhaba wa chakula utokanao na ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
4'29"