Mataifa ridhieni Mkataba wa kufanya kazi na kikosi cha kukomesha utoweshwaji wa binadamu: Guterres
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka manusura na waathirika wa vitendo cha kutoweshwa duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa mataifa yote duniani kuridhia Mkataba na kufanya kazi na Kamati ya Umoja wa Mataifa na Kikosi Kazi cha Kutoweshwa kwa Kulazimishwa.