Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uwajibikaji

Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati MINUSCA  ukihamamsisha wanafunzi kuhusu unyanyasaji wa kingono
UN Photo/Herve Serefio

Kuna hatua katika kupambana na unyanyasaji na ukatili wa kingono UN

Umoja wa Mataifa umeorodhesha visa 259 vya madai ya unyanyasaji na ukatili wa kingono (SEA) mwaka 2018 kwa mujibu wa ripoti mpya ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres iliyowasilishwa leo kwenye Baraza JKuu la Umoja huo. Ingawa idadi ya visa imeongezeka ikilinganishwa na miaka miwli iliyopita , ripoti inaonyesha ongezeko la uelewa miongoni mwa Umoja wa Mataifa na wafanyakazi wanaohusiana na Umoja wa Mataifa , na kumekuwa na nyenzo zilizoboreshwa za kutoa tarifa katika mfumo mzima wa Umoja wa Mataifa.