Chuja:

Utumwa wa kisasa

UN Women/Joe Saad

Utumikishwaji kwenye kazi na kwenye ndoa vyaongezeka

Watu milioni 50 walikuwa wakiishi katika utumwa wa kisasa mwaka jana 2021, kwa mujibu Ripoti ya hivi karibuni ya makadirio ya utumwa wa kisasa duniani ambayo imetolewa na shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa, ILO, Wakfu wa Walk Free na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM. Taarifa inayowasilishwa na Anold Kayanda ina maelezo zaidi. 

Sauti
1'54"

12 SEPTEMBA 2022

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza kwa taarifa ya kwamba utumwa wa kisasa una aina mbalimbali ikiwemo kwenye ajira na pia kwenye ndoa. Kisha anakupeleka kaunti ya Tukrana nchini Kenya ambako UNICEF imenusuru wanawake na mwendo mrefu wa kusaka maji kwa kuwajengea mabwawa ya mchanga. Makala anakukutanisha na Hamad Rashid wa redio washirika MVIWATA FM mkoani Morogoro akikuletea mradi wa UNCDF ambao umekwamua maisha ya wakazi wa Kibondo mkoani Kigoma Tanzania kupitia ushirika wa kilimo uitwao Kibondo Big Power Group.

Sauti
11'48"