WHO kutoa orodha ya vijidudu vinavyoweza kusababisha milipuko ya magonjwa siku zijazo
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limesema linazindua mchakato wa kisayansi wa kimataifa ili kusahihisha orodha yake ya kipaumbele cha vijidudu ambavyo vinaweza kusababisha milipuko ya magonjwa au majanga ya milipuko ya kimataifa ili kuongoza uwekezaji wa kimataifa, utafiti na maendeleo (R&D), hasa katika suala la chanjo, vipimo na matibabu.