Skip to main content

Chuja:

utafiti

Watoto wa kike wang’ara utafiti wa kujua kusoma- UNESCO

Zaidi ya asilimia 96 ya watoto wenye umri wa miaka ya kati ya 9 hadi 10 wanajua kusoma

Ripoti ya utafiti wa zaidi ya nchi 50 duniani uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO umeonyesha kuwa watoto wa kike wanaongoza zaidi kuliko wa kiume.

Nchi ya Urusi imeongoza katika utafiti huo ikifuatiwa na Singapore, Hong Kong, Ireland, Finland na Poland.

Utafiti huo uliofanywa na wataalamu wa UNESCO  kwa kushirikiana na wadau wengine wa elimu ni wa kwanza kufanyika na pia uliangalia kiwango cha kujua kusoma kupitia mitandao.

Demokrasia duniani iko njia panda- Ripoti

Demokrasia duniani iko njia panda na hatua lazima zichukuliwe ili kuilinda na kuiheshimu, imesema ripoti ya kwanza iliyozinduliwa leo huko Geneva, Uswisi kuhusu hali ya demokrasia ulimwenguni.

Ripoti hiyo pamoja na kutambua kuendelea kuchipua kwa demokrasia duniani, pia imeweka bayana kusuasua kwa maendeleo ya demokrasia katika muongo uliopita huku changamoto na vitisho dhidi ya demokrasia vikibainika katika baadhi ya nchi na maeneo.