Wakimbizi wanaume wa Syria wanalawitiwa na kunyanyaswa :UNHCR
Utafiti uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR umebaini kwamba ulawiti, mateso na unyanyasaji wa kingono dhidi ya wanaume na wavulana huenda ni mkubwa zaidi ndani na nje ya Syria kulivyo ilivyodhaniwa hapo awali.