Usonji: Umoja wa Mataifa waadhimisha Siku ya Kimataifa ya Uelewa kuhusu hali hii
Leo tarehe 2 Aprili ni Siku ya Uelewa wa kuhusu Usonji Duniani. Katika tarehe hii, Umoja wa Mataifa huadhimisha michango ya watu wanaoishi na usonji na ulinzi wa haki za kujumuishwa kwa kila mmoja wao.