Usawa na ujumuishwaji kazini ni chachu ya kujenga mnepo na kujikwamua vyema:ILO
Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kazi ulimwenguni, ILO, imebainisha kuwa mtu mmoja kati ya wanne hajisikii kuthaminiwa kazini, huku wale wanaohisi kujumuishwa wakiwa ni wale walioko katika majukumu ya juu zaidi, imeeleza taarifa ya ILO iliyotolewa hii leo mjini Geneva, Uswisi.