Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ushirikiano wa kimataifa

Jarida 28 Septemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo hii leo utasikia shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO na wadau wake wamezindua mkakati wa kwanza wa aina yake wa kutokomeza ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo, ugonjwa ambao unaua mamia ya maelfu ya watu kila mwaka.

pia utasikia taarifa nyingine kuhusiana na nchi ya Jamhuri ya kidemokrasia Kongo - DRC 

Sauti
13'46"
María Fernanda Espinosa Garcés;Rais wa kikao cha 73 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa , akizungumza wakati wa ufunguzi wa mjadala wa wazi wa Baraza hilo
Picha na UN/Cia Pak

Kwa wananchi wa kawaida vitendo ni bora kuliko maneno au hotuba:Espinosa

Maneno matupu na hotuba bila vitendo halisi na hatua zinazoonekana katika kusongesha ajenda ya maendeleo endelevu, havina faida yoyote kwa mwananchi wa kawaida. Hayo yamesemwa leo na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wakati wa ufunguzi wa hafla ya maadhimisho ya kwanza ya siku ya ushirikiano wa kimataifa na amani kwenye makao makuu ya Umoja huo mjini New york Marekani.

 Ufunguzu wa  mkutano wa Mataifa ulifanyika Geneva tarehe 15 Novemba 1920
UN Photo/Jullien

Ushirikiano wa kimataifa ni nguzo kwa dunia na kila mmoja:Guterres

Ushirikiano wa kimataifa na diplomasia vimethibitisha kuwa na faida na huduma muhimu kwa watu wote duniani kuanzia masuala ya utekelezaji wa sheria za kimataifa, usawa wa kijinsia, ulinzi wa mazingira, hadi kuzuia uzalishaji wa silaha za maangamizi na hata magonjwa hatari duniani, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa maadhimisho ya kwanza ya kimataifa hii leo ya “siku ya ushirikiano wa kimataifa na diplomasia kwa ajili ya amani”

UN Photo/Manuel Elías

Guterres:Tunahitaji ushirikiano wa kimataifa sasa kuliko wakati mwingine wowote

Ushirikiano wa kimataifa unahitajika duniani kuliko wakati mwingine wowote ili kukabiliana na changamoto kubwa zinazoikibali dunia hivi sasa kwa pamoja.

Wito huo umetolewa leo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alipozungumza kwenye mjadala wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani kuhusu “kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na jukumu la Umoja wa Mataifa “.

Sauti
3'18"