Skip to main content

Chuja:

usafi

13 Mei 2022

Katika jarida hii leo utasikia wito wa kusaidia wakulima wa Somalia ili kuiokoa nchi isiingie katika janga kubwa la kibinadamu. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC linatumia wafanyakazi wa kijamii kuhamasisha wakazi wa vitongoji vya mji mkuu, Kinshasa kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona, au COVID-19 kwa kuwa baadhi ya watu bado wanasuasua kupatiwa chanjo hiyo.

Wananchi wa Turkana Kenya wamepaaza sauti ya madhila yanayowasibu na UNICEF kueleza nini wanafanya kusaidia katika eneo la usafi na kujisafi. 

Sauti
12'58"

Choo chako ni salama?

Utafiti umebaini kwamba ukosefu wa vyoo safi  na salama ni hatarishi kwa afya ya binadamu. Takwimu za mashirika ya ufya ulimwenguni kama WHO na wengine zinaonyesha kuwa jamii zinazoishi katika mazingira yasiyo na vyoo salama zipo katika athari za kupatwa na milipuko ya magonjwa yatokanayo ya ukosefu wa matumizi salama ya vyoo kama kipindupindu na magonjwa mengine.