UN yatoa onyo vita Ukraine viko katika zama hatari zaidi kwa raia
Miaka mitatu na nusu tangu uvamizi kamili wa Urusi, vita vya Ukraine vimeingia katika hatua hatari na ya vifo zaidi kwa raia, amesema leo Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa.
Miaka mitatu na nusu tangu uvamizi kamili wa Urusi, vita vya Ukraine vimeingia katika hatua hatari na ya vifo zaidi kwa raia, amesema leo Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa.
Urusi imetumia sehemu ya hotuba yake ya leo kwenye mimbari ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuzungumzia hatua ya nchi za magharibi kupinga ndani ya Baraza la Usalama pendekezo la kuiongezea muda Iran nafuu ya vikwazo kwa mujibu wa makubaliano ya mwaka 2015.
Baraza la Usalama na Umoja wa Mataifa leo limeitisha kikao cha dharura kufuatia uvunjaji wa Urusi wa sheria za anga ya Estonia. “Ukiukaji wa sheria za anga za nchi huru haukubaliki.” Kauli hii ilitolewaleo kwenye kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu, Miroslav Jenča. Sababu ya kikao hicho ni tukio lililotokea Septemba 19, ambapo, kwa mujibu wa Estonia, ndege tatu za kivita aina ya MiG-31 za Urusi zilivunja sheria na kuingia katika anga yake.
Alasiri ya Ijumaa Septemba 12, 2025, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kwenye kikao cha dharura kilichoitishwa na Poland kuhusu ndege zisizo na rubani za Urusi zilizorushwa na taifa hilo la Ulaya Mashariki kuelekea maeneo ya Belarus na hatimaye kuingia anga la Poland usiku wa kuamkia leo.
Umoja wa Mataifa umelaani vikali shambulio la Urusi lililotokea lililofanyika leo katika kijiji cha Yarova, mkoa wa Donetsk, ambalo limeua zaidi ya watu 20 na kuwajeruhi karibu wengine 20.
Mtoto mchanga ni miongoni mwa waliouawa usiku wa kuamkia Jumapili ya Septemba 8 katika kile kilichoripotiwa kuwa shambulio kubwa la anga la Urusi dhidi ya Ukraine tangu uvamizi wake wa mwaka 2022 uanze kwa ukubwa.
Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Urusi nchini Ukraine yaliyofanyika usiku kucha, ikiwemo katika miji ya Kharkiv na Zaporizhzhia, yameripotiwa kuua watu 10 wakiwemo watoto watatu, kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa leo. Flora Nducha na taarifa zaidi
Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Urusi nchini Ukraine yaliyofanyika usiku kucha, ikiwemo katika miji ya Kharkiv na Zaporizhzhia, yameripotiwa kuua watu 10 wakiwemo watoto watatu, kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa leo.
Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (drones) na makombora yaliyofanywa na jeshi la Urusi dhidi ya mji mkuu wa Ukraine, Kyiv, usiku wa kuamkia leo yameelezewa na Umoja wa Mataifa kama “mashambulio ya vifo zaidi kuwahi kutokea katika jiji hilo katika kipindi cha karibu mwaka mmoja.”
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki IAEA, Rafael Mariano Grossi, amewasilisha taarifa kali kwa Bodi ya Magavana ya shirika hilo leo, akieleza wasiwasi mkubwa kuhusu kushindwa kwa Iran kushirikiana ipasavyo na wakaguzi wa nyuklia.