22 MEI 2023
Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya ukatili wa kijinsia nchini DRC na msaada wa kibinadamu nchini Myanmar. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunakupeleka Ureno, kulikoni?
Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya ukatili wa kijinsia nchini DRC na msaada wa kibinadamu nchini Myanmar. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunakupeleka Ureno, kulikoni?
Mwenyekiti mwenza wa Mkutano wa Pili kuhusu Bahari unaofanyika huko Lisbon, Ureno Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametaka vijana kuwa kiti cha mbele katika mashauriano yoyote kuhusu mustakabali wa bahari.
Mkutano wa pili wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari umeanza leo huko Lisbon Ureno ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ni lazima kubadili mwelekeo na mwenendo wa shughuli za binadamu kwa bahari la sivyo uchafuzi wa bahari utavuruga harakati zote za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Ndivyo alivyokuwa anatamatisha hotuba yake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo huko Lisbon kwa lugha ya kiswahili kwenye mkutano huo wa baharí ulioandaliwa kwa pamoja na Kenya na Ureno.
Tukiwa bado kwenye mkutano huo wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari, mbali ya kikao cha ngazi ya juu cha viongozi makundi mbalimbali yalianza kukutana mwishoni mwa wiki likiwemo kongamano la vijana.
Dunia lazima ifanye jitihada zaidi ili kukomesha kuzorota kwa hali ya afya ya bahari, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo Jumapili, akiwataka vijana waliokusanyika Carcavelos, Ureno, kwa ajili ya jukwaa la vijana na ubunifu la Umoja wa Mataifa kuongeza kasi kwa sababu viongozi wa kizazi chake wanasuasua.
Hakuna shaka kwamba utupaji na upotevu wa chakula, umekuwa ukidhoofisha uendelevu wa mifumo yetu ya chakula. Katika jitihada za kukabiliana na hili, baadhi ya makampuni ya biashara ndogo ndogo duniani kote yanaweka mkazo katika mbinu mpya endelevu za usimamizi wa taka.
Bahari ndiyo mfumo mkubwa zaidi wa ikolojia wa sayari dunia, unaodhibiti hali ya hewa, na kutoa uwezo wa maisha kwa mabilioni ya watu.
Siku ya bahari duniani ikiadhimishwa hii leo, macho na masikio yanaelekezwa huko Lisbon, Ureno ambako kuanzia tarehe 27 mwezi huu hadi tarehe 1 mwezi Julai kutafaniyka mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari.
Nataliia Vladimirova alikimbia nyumbani kwake Kharkiv, Ukraine, siku ya kwanza tu Urusi ilipovamia nchi yao tarehe 24 mwezi Februari, 2022, akiambatana na binti yake Oleksandra mwenye umri wa miaka 4 pamoja na mama mkwe wake. Wao ni miongoni mwa maelfu ya wakimbizi wa Ukraine waliopata hifadhi ya muda nchini Ureno . Akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa huko Ureno, Nataliia al maaruf Natasha, anasimulia simulizi wa yale aliyopitia ikiwemo kugawanyika kwa familia sambamba na kupoteza wengine.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema huu ni wakati wa mabadiliko , na kizazi chacke kimeanza kuelewa kwamba vijana wanaweza na wanapaswa kushika usukani .