Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UNWTO

21 SEPTEMBA 2020

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea 

-Umoja wa Mataida waadhimisha miaka 75 tangu kuanzishwa mkuu wa Umoja huo asema pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana safari bado ni ndefu inayohitaji mshikamano kunusuru kizazi hiki na vijavyo

-Tanzania inasema katika miaka 75 ya Umoja wa Mataifa kumekuwa na ushirikiano mkubwa na mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa ikiwemo la maendeleo UNDP, na la utalii UNWTO utamsikia Devotha Mdachi kutoka bodi ya utalii Tanzania

Sauti
14'51"

Idadi ya watalii duniani ilipanda 2017 na huenda ikaongezeka zaidi :UNWTO

Idadi ya watalii wa kimataifa, wanaowasili katika nchi nyingine, na watu wanaoingia nchi moja kwa siku kwa njia  halali iliongezeka mwaka wa 2017 kwa kiwango cha asili mia 7 na na hivyo  kufikia watalii Zaidi ya millioni elfu moja na mia tatu.

Hii ni kwa mujibu wa vigezo vipya vya shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii duniani UNWTO. Shirika hilo linabashiri kuwa ongezeko hilo litazidi kuvuma mwaka 2018 kwa kiwango cha asili mia  kati ya nne na tano.