Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UNODC

UN News

Mradi wa PLEAD wawezesha huduma za mahamaka kupatikana muda wote nchini Kenya

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNDOC kanda ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na sekta ya mahakama nchini kenya wamepanga kuanza kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa uwekaji umeme wa sola katika mahakama na magereza nchini humo baada ya awamu ya kwanza kuonesha mafanikio.

Kupitia mradi ujulikanao kama PLEAD unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya UNODC na sekta ya mahakama nchini Kenya wamefanikiwa kutekeleza mradi wa awamu ya kwanza katika mahakama mbili zilizoko Mombasa ambazo zilikuwa zikishindwa kuendesha shughuli zake pindi umeme unapokatika.

Sauti
3'23"

16 DESEMBA 2022

Jaridani leo Ijumaa ya tarehe 16  ya mwezi Desemba mwaka 2022 tunakuletea habari kuhusu uhamiaji na kazi za walinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.  

Sauti
11'31"
Uchunguzi wa polisi katika nchi zilizoendelea ni muhimu katika kukabiliana na uhalifu wa kimataifa wa kupangwa
UN Photo/Martine Perret

Wahalifu wanasaka kufaidika na COVID-19, tushirikiane kupambana nao:UNODC 

Wakati mitandao ya uhalifu kote duniani ikijaribu kusaka mbinu za kunufaika na janga la corona au COVID-19, ni muhimu kwa serikali kushirikiana na kufanyakazi pamoja kwa mujibu wa mktaba wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na usafirishaji haramu wa binadamu, usafirishaji wa silaha na uhalifu miongoni mwa nchi , amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres. 

08 JULAI 2020

Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

-Janga la COVID-19 laongeza usafirishaji haramu wa vifaa tiva visivyokidhi viwango au bandia duniani imesema ripoti iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNODC

-Nchini Sudan Kusini wapiganaji wa makundi mbalimbali walioletwa pamoja ili kujiunga na mafunzo ya kuingia katika jeshi la kitaifa karibu wanahitimu

Sauti
12'23"