Ukatili na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu umetekelezwa Unity:OHCHR/UNMISS
Ripoti ya pamoja ya haki za binadamu iliyochapishwa leo na ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) na Ofisi ya kamishna mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa (OHCHR) imeaanisha ukatili na ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa za haki za binadamu na ubinadamu kwenye jimbo la Unity Sudan Kusini.