Watoto takriban 490,000 wameathirika na mafuriko makubwa nchini Sudan Kusini limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF na kuongeza kuwa mvua kubwa zilizoanza kunyesha tangu mwezi Julai mwaka huu zimeathiri jumla ya watu 908,000 katika kaunti 32.