Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UNIC Dar es salaam

Warren Bright/UNFPA Tanzania

Waandishi wa habari nao wapata elimu kuhusu SDGs Tanzania

Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam kimewaelimisha waandishi wa habari wa Morogoro Tanzania kuhusu Malengo ya maendeleo endelevu. Kupitia makala hii iliyoandaliwa na Ahimidiwe Olotu, Stella Vuzo wa Kituo hicho cha habari cha Umoja wa Mataifa anaanza kwa kueleza nia ya mafunzo.

Sauti
2'57"
UN News/Elizabeth Scaffidi

Umoja wa Mataifa una fursa nyingi, muhimu vijana tuwe tayari na tuwe na moyo wa kujitolea-Hilda Phoya

“Umoja wa Mataifa una fursa nyingi ambazo ikiwa vijana tutakuwa na moyo wa kujitolea na bidii ya kazi, tunaweza kunufaika nazo,” hayo ni maoni ya Hilda Phoya, mwanafunzi ambaye hivi karibuni amehitimisha mafunzo kwa vitendo katika Kituo cha habari za Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam Tanzania. 

Katika mahojiano haya yaliyofanywa na Ahimidiwe Olotu wa Kituo hicho, Hilda anaanza kwa kueleza kilichomvutia kuchagua kwenda katika kituo hicho ili kukamilisha masomo yake ya elimu ya juu. 

Sauti
3'7"
Hilda Phoya, mnufaika wa mafunzo kwa vitendo katika ofisi za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania.
UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Umoja wa Mataifa una fursa nyingi, muhimu vijana tuwe tayari na tuwe na moyo wa kujitolea-Hilda Phoya

“Umoja wa Mataifa una fursa nyingi ambazo ikiwa vijana tutakuwa na moyo wa kujitolea na bidii ya kazi, tunaweza kunufaika nazo,” hayo ni maoni ya Hilda Phoya, mwanafunzi ambaye hivi karibuni amehitimisha mafunzo kwa vitendo katika Kituo cha habari za Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam Tanzania. 

Sauti
3'7"
UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Asante UNIC Dar es Salaam kunipa fursa ya kukuza maarifa yangu-Hilda Amedhastone Phoya

Je una ndoto za siku moja kufanya kazi na Umoja wa Mataifa? Makala ifuatayo ni mahojiano kati ya Ahimidiwe Olotu wa UNIC Dar es Salaam na Hilda Amedhastone Phoya, mwanafunzi ambaye amehitimisha mafunzo kwa vitendo katika Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam, akieleza kuhusu alivyonufaika na fursa ya kujifunza kwa vitendo katika kituo hicho kinachohusika na habari za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na jinsi kituo hicho kilivyonoa uelewa wake kuhusu masuala mbalimbali ya kimataifa. 

Sauti
3'39"
Shughuli za ununuzi kwenye duka jijini Dar es Salaam, Tanzania wakati huu ambapo kumeripotiwa kutangazwa kwa visa vya corona nchini humo.
UN News/ Stella Vuzo

Tanzania inavyokabili janga la corona

Ni miezi miwili na zaidi sasa tangu Tanzania itangaze mgonjwa wake wa kwanza wa virusi vya COVID-19.  Tangu tarehe 16 mwezi wa tatu mwaka huu mengi yamejiri nchini Tanzania kufuatia kuzuka kwa janga la ugonjwa huo unaoathiri dunia nzima.

UNICEF/Tapash Paul

Mapendekezo ya UNICEF Tanzania katika kuimarisha elimu ya awali

Hii leo katika makala tunaendelea na sehemu ya pili ya mahojiano kati ya Stellla Vuzo wa kituo cha habari za Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es Salaam nchini Tanzania na Audast Muhinda, afisa kitengo cha elimu katika shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF ambapo Bwana Muhinda anatoa mapendekezo yake katika kuhakikisha kwamba idadi ya watoto wanaopokea elimu ya awali inaongezeka.

Sauti
3'50"
UN SDGs

SDGs zahitaji kuelewa ndipo zitekelezeke:Muzenda

Ikiwa imesalia miaka 11 kuelekea mwaka 2030 ambao ndiyo umepangwa na Umoja wa Mataifa kuwa mwaka ambao malengo ya maendeleo endelevu, SDGs yatakuwa yametimizwa, Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wameendelea kuhamasisha umma kwanza kuyafahamu malengo yenyewe na pia kuyatekeleza. Miongoni mwa wadau hao ni Munyaradzi Muzenda kutoka Zimbabwe ambaye ni mkurugenzi wa taasisi ya Africa Speaks, yeye anaendesha kampeni ya kukuza uelewa kuhusu SDGs, Arnold Kayanda na maelezo zaidi.

Sauti
2'8"
Wachechemuzi wa malengo endelevu, SDGs yaliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa 2015
UN SDGs

Tunakusudia kuyapandisha malengo ya maendeleo endelevu kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro-Munyaradzi Muzenda

Ikiwa imesalia miaka 11 kuelekea mwaka 2030 ambao ndiyo umepangwa na Umoja wa Mataifa kuwa mwaka ambao malengo ya maendeleo endelevu, SDGs yatakuwa yametimizwa, Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wameendelea kuhamasisha umma kwanza kuyafahamu malengo yenyewe na pia kuyatekeleza. Miongoni mwa wadau hao ni Munyaradzi Muzenda kutoka Zimbabwe ambaye ni mkurugenzi wa taasisi ya Africa Speaks, yeye anaendesha kampeni ya kukuza uelewa kuhusu SDGs, Arnold Kayanda na maelezo zaidi.

Sauti
2'8"
UN

Natumia uelewa wangu kuhusu mauaji ya halaiki kuepusha yasiyotokee tena- Mwanafunzi Tanzania

Miaka 74 tangu kukombolewa kwa kambi ya mateso na mauaji ya wayahudi milioni Sita huko  Auschwitz-Birkenau, nchini Poland yaliyofanywa na manazi wa Ujerumani, bado kuna ubaguzi kwa misingi mbalimbali iwe ya kidini au kikabila. Hali hii  hutia sana wasiwasi Umoja wa Mataifa ambao uliamua siyo tu kutenga siku ya kimataifa ya kumbukizi ya mauaji hayo ya halaiki dhidi ya wayahudi kama fursa ya kukumbuka na kutathmini, bali pia kuwa na programu maalum ya kuelimisha jamii juu ya madhila ya mauaji ya aina hiyo na viashiria vyake ili kuepusha yasitokee tena.

Sauti
4'5"