Umoja wa Mataifa umeisihi Ugiriki iboreshe mazingira na kasi ya mapokezi ya wasaka hifadhi kwenye mkoa wa Evros ambako wakimbizi wanazidi kumiminika wakipitia mpaka wa nchi hiyo na Uturuki.
Kuimarika kwa hali ya usalama jimboni Darfur nchini Sudan kumesababisha awamu ya kwanza ya wakimbizi waliosaka hifadhi nchini Chad kurejea jimboni humo wiki hii.
Umoja wa Mataifa una wasiwasi mkubwa juu ya madhila yanayokumba wahamiaji, wasaka hifadhi na wakimbizi wapya nchini Yemen. Yaelezwa manusura hufyatuliwa risasi, hupigwa kila mara, hubakwa na hata huvuliwa nguo na kusalia uchi.
Umoja wa Mataifa umejionea miradi dhahiri ya kilimo, ufugaji na biashara inayotekelezwa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kwa ajili ya kuwajengea uwezo wakimbizi wanaotoka nchi jirani.
Idadi kubwa ya wakimbizi wa Burundi wanahofiwa kufariki dunia baada ya mabasi walimokuwa wakisafiria kurejea nyumbani kutoka Tanzania kupata ajali mkoani Kagera, kaskazini-magharibi mwa Tanzania.
Maelfu ya wakimbizi wa Ethiopia wanaohifadhiwa nchini Kenya hivi sasa wanakabiliwa na mtihani mkubwa wa kukidhi mahitaji yao ya msingi kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limeshtushwa na ongezeko la idadi ya wakimbizi wa Cameroon wanaosaka hifadhi Nigeria ambapo idadi yao sasa imefikia 20,000.