Skip to main content

Chuja:

UNGA77

Csaba Kőrösi (kushoto) Rais wa mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la UN akikabishi rungu la kuongoza mkutano kwa Rais wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la UN (UNGA78). Kulia kabisa ni Naibu Katibu Mkuu wa UN Amina J. Mohammed
UN /Manuel Elias

UNGA 77 yafunga pazia, Rais wa UNGA78 ala kiapo

Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umekunja jamvi asubuhi ya tarehe 5 Septemba 2023, jijini New York, Marekani kwa Rais wa mkutano huo anayemaliza muda wake Csaba Kőrösi akisisitiza kuwa licha ya mikingamo ya kijiografia, ushirikiano baina ya nchi haukwepeki.

06 OKTOBA 2022

Hii leo katika Habari za UN Assumpta Massoi anakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Kujifunza Lugha ya Kiswahili.

Katika Habari kwa Ufupi kuna haki za mtoto kuzingatiwa hasa wakati huu ambapo majanga ya kiasili na yanayosababishwa na binadamu  yanakengeua utekelezaji wa haki za mtoto. Suala la afya ya akili barani Afrika ambayo inachochea matukio ya kujiua ,na WHO imezindua kampeni maalum. Na kisha ni uzinduzi wa ripoti kuhusu matumizi ya matukio makubwa ya michezo ili kuimarisha afya ya mwili ya binadamu.

Sauti
11'26"
Taswira ya ukumbi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
UN Photo/Manuel Elías

UNGA77 yafunga pazia, Afrika yasema sasa ni wakati wa kuwa na ujumbe wa kudumu

Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA77 umekunja jamvi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa ukiwa na maudhui: Wakati muhimu: Majawabu ya kuleta marekebisho kwa changamoto zinazofungamana. Katika siku 6 za mjadala huo nchi za Afrika zilitumia fursa kuhoji marekebisho gani yanawezekana bila kurekebisha chombo hicho ambacho kura  yenye maamuzi ya msingi inamilikiwa na wanachama 5 kati ya 193, ikiwa ni miaka 77 tangu kuudwa kwake.

27 Septemba 2022

Hii leo katika Habari za UN Flora Nducha anakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa kina na Mashinani.

Katika Habari kwa ufupi: Kurejea nyumbani kwa hiyari kwa wakimbizi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kutoka nchini Zambia. Pili kutangazwa kutokomezwa kwa EBola nchini DRC na Habari ya Tatu ni kuhusu siku ya utalii duniani na wito kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kutaka utalii wa aina mpya usioaharibu mazingira na wenye mnepo kwa kila mkazi wa dunia.

Sauti
13'48"
Csaba Kőrösi  Rais wa UNGA77 akiendesha mjadala wa wazi wa Baraza Kuu katika siku ya mwisho ya mjadala huo
UN Photo/Cia Pak

Körösi, akunja jamvi la mjadala wa ngazi ya juu wa UNGA77

Magari yaliyotanda kuzunguka makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuhakikisha usalama wakati wa wiki ya mjadala wa ngazi ya juu wa viongozi kwenye Baraza Kuu UNGA77 sasa yameondoka na barabara iliyofungwa kufunguliwa, polisi wengi na maafisa wa ujasusi ambao walizuia njia za kuelekea kwenye jengo la Umoja wa Mataifa, nao wametrejea kwenye majukumu yao ya kila siku, kilomita za vyuma vilivyokuwa vizuizi kuzunguka eneo hilo la Umoja wa Mataifa New York, vinavyojulikana kama Turtle Bay navyo vimesafirishwa kwa malori hadi kwenye maghala kusubiri hadi mwakani kwani wiki ya mjadala wa ngazi ya juu imemalizika kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  .