Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UNGA75

1 Oktoba 2020

Hii leo mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA75 unakuwa na kikao cha ngazi ya juu kuhusu kuchagiza utekelezaji wa usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake na mtoto wa kike, sambamba na maadhimisho ya miaka 25 tangu mkutano wa 4 wa kimataifa kuhusu wanawake uliofanyika Beijing nchini China mwaka 1995. 

Changamoto kwangu ni fursa ya kujifunza asema Fiona Beine mlinda amani raia wa Uganda nchini Iraq.

Wazee lazima wawe kipaumbele katika juhudi zetu za kuishinda COVID-19-Guterres  

Sauti
13'32"
UN Webccast

Misaada ya kimkakati ni muhimu ili kukwamua nchi zilizotwama kutokana na COVID-19: Tanzania

Tanzania imezungumza kwenye mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuelezea msimamo wake katika masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano wa kimataifa, janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19, amani na usalama maziwa makuu na mustakabali wa Umoja wa Mataifa wakati huu ambapo chombo hicho kinatimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake.

Sauti
2'59"
Balozi Philip Ochen Odida, Naibu Mwakilishi wa kudumu wa Uganda katika Umoja wa Mataifa akihutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA75
UN Photo/Loey Felipe

COVID-19 imetupa mafunzo-Uganda 

Tunauona ushirikiano wa kimataifa kama njia ya kushughulikia matishio magumu na mapya kama vile janga la COVID-19 ambalo limeathiri kila mwanachama wa jumuiya ya kimataifa, imeeleza sehemu ya kwanza ya hotuba ya Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda katika mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambayo imesomwa kwa niaba yake na Naibu Mwakilishi wa kudumu wa Uganda katika Umoja wa Mataifa, Balozi Philip Ochen Odida ikieleza pamoja na mengine, kile ambacho wamejifunza kutokana na ugonjwa huo. 

Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Kennedy Gastorn akihutubia Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo Jumanne Septemba 29, 2020
UN /Loey Felipe

Tunashukuru kwa usaidizi dhidi ya COVID-19, sasa maisha yamerejea hali ya kawaida- Tanzania

Tanzania imezungumza kwenye mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuelezea msimamo wake katika masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano wa kimataifa, janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19, amani na usalama maziwa makuu na mustakabali wa Umoja wa Mataifa wakati huu ambapo chombo hicho kinatimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake.
 

Sauti
2'59"