Baraza Kuu lakutana kumuenzi Hayati Magufuli
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na kikao rasmi cha kumuenzi na kumkumbuka Rais wa 5 wa Tanzania Dkt. John Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi uliopita.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na kikao rasmi cha kumuenzi na kumkumbuka Rais wa 5 wa Tanzania Dkt. John Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi uliopita.
Mwaka 2020 ulikuwa ni mwaka wa majanga lakini 2021 ni mwaka wa fursa na matumaini! Ni kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyotoa leo kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani akielezea vipaumbele vyake 10 kwa mwaka 2021.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amehutubia mkutano wa kuadhimisha miaka 75 tangu mkutano wa kwanza wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ulipofanyika mjini London Uingereza.
Janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19 likiendelea kutikisa duniani, Umoja wa Mataifa hii leo umeanza kikao maalum cha ngazi ya juu cha siku mbili kujadili janga hilo ambalo hadi sasa limesababisha vifo vya watu zaidi ya 1,400,000 duniani kote.
Tanzania imeteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hati za Utambulisho ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, New York, kwa mwaka 2020/2021.
Hii leo mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA75 unakuwa na kikao cha ngazi ya juu kuhusu kuchagiza utekelezaji wa usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake na mtoto wa kike, sambamba na maadhimisho ya miaka 25 tangu mkutano wa 4 wa kimataifa kuhusu wanawake uliofanyika Beijing nchini China mwaka 1995.
Changamoto kwangu ni fursa ya kujifunza asema Fiona Beine mlinda amani raia wa Uganda nchini Iraq.
Wazee lazima wawe kipaumbele katika juhudi zetu za kuishinda COVID-19-Guterres
Wakati mjadala wa kihitoria wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitia mtandaoni UNGA75 umefunga pazia leo, Rais wa Baraza Kuu la Umoja huo amesema viongozi wa kisiasa wameahidi kuonesha mshikamano wa kimataifa.
Tanzania imezungumza kwenye mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuelezea msimamo wake katika masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano wa kimataifa, janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19, amani na usalama maziwa makuu na mustakabali wa Umoja wa Mataifa wakati huu ambapo chombo hicho kinatimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake.
Tunauona ushirikiano wa kimataifa kama njia ya kushughulikia matishio magumu na mapya kama vile janga la COVID-19 ambalo limeathiri kila mwanachama wa jumuiya ya kimataifa, imeeleza sehemu ya kwanza ya hotuba ya Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda katika mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambayo imesomwa kwa niaba yake na Naibu Mwakilishi wa kudumu wa Uganda katika Umoja wa Mataifa, Balozi Philip Ochen Odida ikieleza pamoja na mengine, kile ambacho wamejifunza kutokana na ugonjwa huo.
Tanzania imezungumza kwenye mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuelezea msimamo wake katika masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano wa kimataifa, janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19, amani na usalama maziwa makuu na mustakabali wa Umoja wa Mataifa wakati huu ambapo chombo hicho kinatimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake.