Baraza Kuu la UN lathibitisha uteuzi wa Bi. Inger Andersen kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa UNEP
Kufuatia pendekezo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, baada ya kushauriana na Nchi Wanachama, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limemthibitisha Inger Andersen raia wa Denmark kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Mazingira (UNEP) kwa muhula mwingine wa miaka minne kuanzia tarehe 15 Juni 2023 hadi 14 Juni 2027.