Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UNEP

Inger Andersen, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP), akizungumzia tukio la Ripoti ya Pengo la Uzalishaji katika mkutano wa COP27, huko Sharm El-Sheikh, Misri.
© UNFCCC/Kiara Worth

Baraza Kuu la UN lathibitisha uteuzi wa Bi. Inger Andersen kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa UNEP

Kufuatia pendekezo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, baada ya kushauriana na Nchi Wanachama, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limemthibitisha Inger Andersen raia wa Denmark kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Mazingira (UNEP) kwa muhula mwingine wa miaka minne kuanzia tarehe 15 Juni 2023 hadi 14 Juni 2027.

UN News

Asante Katibu Mkuu kwa kuendelea kuniamini: Elizabeth Mrema

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres Jumanne wiki hii alimtangaza Elizabeth Maruma Mrema kutoka nchini Tanzania kuwa naibu mkurugenzi mtendaji mpya wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP. 

Bi Mrema tangu mwaka 2020 amehudumu kama katibu mtendaji wa sekretarieti ya mkataba wa Umoja wa Mataifa wa bayoanuai CBD, yenye makao yake makuu mjini Montreal, Canada akizungumza na Idhaa hii ya Kiswahili baada ya uteuzi huo ameelezea alivyoupokea 

(SAUTI YA ELIZABETH MREMA) 

Sauti
2'37"
© UNICEF/Lamek Orina

Ukame Kenya: Serikali imeanza mchakato wa kufadhili Mfuko wa Taifa wa Dharura lakini tunahitaji usaidizi kuokoa maisha ya watu

Umoja wa Mataifa na wadau wake wa masuala ya kibinadamu nchini Kenya wameomba dola milioni 472.6 kusaidia watu milioni 4.3 walioathiriwa na ukame, ili kuunga mkono mwitikio unaoongozwa na Serikali, huku janga hilo likitarajiwa kuwa mbaya zaidi. Hali katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo katika Pembe ya Afrika, ni mbaya. Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gachagua anaeleza kuwa mzigo huu wa janga la mabadiliko ya tabianchi ni mkubwa kwa nchi yake na kwa hivyo ni muhimu jumuiya ya kimataifa ikasaidia lengo hilo la Umoja wa Mataifa kwani hali ya wananchi inazidi kuwa mbaya.

Sauti
5'6"

04 JUNI 2021

Katika jarida la mada kwa kina kutoka Umoja wa Mataifa hii leo Leah Mushi anakuletea:

-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema mashambulizi makali yanayotekelezwa na wapiganaji wa kundi la Allied Democratic Forces ADF, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC yamewalazimisha takriban watu 5,800 kukimbia mara kadhaa katika makazi ya watu waliotawanywa katika jimbo la Ituri Mashariki mwa nchi hiyo

Sauti
12'19"