Chuja:

UNEA

02 MACHI 2022

Katika jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Leah Mushi anakuletea

-Idadi ya watu waliokimbia mashambulizi nchini Ukraine katika kipindi cha siku 6 zilizopita ni zaidi ya 870,000, limesema hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, kupitia jukwaa lake lililozindua ili kuonesha takwimu za watu wanaokimbia wakiwemo raia na wageni. 

Sauti
11'29"

22 Februari 2021

U hali gani siku ya leo Jumatatu Februari 22 mwaka 2021 na mwenyeji wako Flora Nducha anakueletea mada kwa kina akimulika lugha ya mama, kwa kuzingatia kuwa tarehe 21 mwezi Februari ni siku ya lugha ya mama duniani. Katika kutekeleza hilo Grace Kaneiya akiwa Nairobi, Kenya amefuatilia wito kwa watunga sera, waelimishaji na walimu, wazazi na familia kuimarisha dhamira zao katika kuhakikisha elimu kupitia lugha mbali mbali na ujumuishaji kati elimu ili kuibuka kutokana na athari za janga la virusi vya Corona au COVID-19.

Sauti
11'7"