Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UNDP Tanzania

Mohamed Nasser

Umeme wa sola washika kasi Tanzania,  UNDP yaonyesha njia

Lengo namba 7 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs yaliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 2015, yanataka pamoja na mambo mengine kuhakikisha nishati ya kisasa iliyo nafuu na ya uhakika inapatikana ili kufanikisha shughuli za kila siku za maendeleo. Nchini Tanzania Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la mpango wa maendeleo, UNDP limeamua kuonyesha njia kuwa hilo linawezekana kwa kuwa kuwekeza kwenye sola mwanzoni ni gharama lakini ni gharama inayopunguza gharama za usoni.

Sauti
4'10"

Njombe wafurahia usaidizi wa UN

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo, UNDP Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na wadau wengine wa maendeleo kutoka Uingereza, Marekani na Sweden  na serikali ya Tanzania linajitahidid kutekeleza mpango wa kunusuru kaya masikini (PSSN) kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), ambao kwa sasa umefikia takriban kaya milioni 1.1 wenye umasikini uliokithiri nchini humo...

Sauti
3'31"